Matokeo
Re-Forma imetengeneza matokeo kadhaa yanayoonyesha tunachosadiki kwamba wachungaji wanahitaji kujua, kufanya na kuwa. Watoa huduma wenye mtaala wanaweza kukamilisha matokeo yao na yoyote ambayo hawajafanya orodha hapa chini, wakati watoa huduma wapya watafanya yote. Wanafunzi wanahitaji kuonyesha walifanikisha matokeo yote kabla ya kupewa Cheti cha Mafunzo ya Biblia kwa Huduma.
Matokeo ya Re-Forma yanapatikana bila malipo kwa mtoa huduma yeyote anayetaka wanafunzi wake wafuzu Cheti cha Re-Forma, kinachosaidiwa na Muungano wa Kimataifa wa Kiinjili. Tafadhali kumbuka kwamba hii si programu iliyoidhinishwa, lakini Cheti kinatoa kiwango cha kimataifa kwa mafunzo yasiyo rasmi. Ikiwa wanafunzi wameonyesha matokeo yote, watakuwa na sifa moja kwa moja.
Utoaji wa Cheti utagharimu ada ya utawala ya $5 US kwa kila mwanafunzi, pamoja na ada ya ujumbe, katika nchi zinazoendelea na $10 kwa kila mwanafunzi pamoja na ada ya ujumbe mahali pengine. Tafadhali kumbuka kwamba hakuna vyeti vitakavyotolewa bila malipo ya awali.
Utapata rasilimali za kusaidia kwa matokeo mengi chini ya kichupo cha Viungo Muhimu.
Muhimu! Katika hali zote, wanafunzi lazima waweze kutumia walichojifunza katika muktadha wao. Tafadhali tuma Karatasi ya Tathmini iliyokamilika kwa kila mwanafunzi mwishoni mwa programu kwa anwani iliyotolewa kwenye Karatasi ya Tathmini.
Matokeo yote yanaanza na "Wanafunzi wataweza …"
1. Kuongoza kama Yesu
- Zaa tunda la Roho katika nyanja zote za maisha na kuuishi unyenyekevu, uadilifu na usahili (kutokujifanya)
- Kuorodhesha, kueleza na kufanyia kazi mambo ya kiroho.
- kueleza na kuonyesha kanuni 5 muhimu, za kibiblia za maombi kama msingi wa huduma zote.
- kueleza kanuni za ibada ya kibinafsi na ya ushirika na kueleza jinsi ya kuzitekeleza kama mtindo wa maisha.
- Kutumia kanuni za kimaadili za kibiblia katika mahusiano kanisani au kwenye huduma.
- Kueleza jinsi mtazamo wa Yesu juu ya wanawake na watoto unapaswa kulibadilisha kanisa.
- Kueleza msingi wa kibiblia wa uwakili wa muda, uwezo, rasilimali, na uumbaji.
- Kueleza umuhimu wa kanisa.
- ueleza msingi wa kibiblia wa ubatizo na Meza ya Bwana.
- Kueleza jinsi ya kupanga na kusimamia kanisa au huduma kwa ubora na uadilifu.
- Kueleza jinsi nguvu za Kristo zinavyoshinda tamaa ya mwili, ya ulimwengu na ya ibilisi.
2. Kulitumia Neno
- Kueleza 'Simulizi kuu' ya Biblia nzima pamoja Yesu akiwa katikati ya mpango wa Mungu wa wokovu.
- Kutambulisha vitabu 3 katika kila aina ya uandishi katika Biblia kwa kubainisha mwandishi, kipindi, madhumuni na aina ya uandishi.
- Kufanya muhtasari wa angalau mafundisho makuu 5 ya Yesu.
- Kueleza umuhimu wa kifo na ufufuka kwa Yesu.
- Kueleza matukio makuu 5 katika kitabu cha Matendo ya mitume.
- Kuandaa na kuhubiri au kufundisha Neno la Mungu kwa ufanisi.
- Amini, eleza na kuweka katika matendo mafundisho muhimu ya Biblia.
- Kueleza ni kwa namna gani "injili ya mafanikio" si ya kibiblia na si ya kimaadili.
- Onyesha mtazamo wa ulimwengu wa kibiblia ulivyo juu ya mitazamo mbadala ya ulimwengu katika muktadha wao.
- Eleza matukio 3 muhimu, kila moja kutoka kwa kipindi tofauti katika historia ya Kanisa.
- Eleza mizizi ya kihistoria ya madhehebu yao (au harakati za kanisa).
3. Kuwafikia na Kuwafanya Wanafunzi
- Shirikisha injili kwa ufanisi kwa familia, marafiki na wageni.
- Kuhamasisha na kushawishi wengine kwa ajili ya utume wa Mungu.
- Mwongoze angalau mtu mmoja katika aina maalum ya uinjilisti au utume.
- Eleza jinsi wanaweza kutekeleza kielelezo cha Yesu cha kufanya wanafunzi.
- Tambua na uwafundishe angalau watu wengine watatu kuhudumu katika aina fulani ya huduma ya kanisa.
- Eleza jinsi Biblia inavyopaswa kuhusiana na kutafsiri utamaduni katika muktadha wao.
- Tumia teknolojia na mitandao ya kijamii kwa makusudi katika huduma.
4. Kuchunga Watu wa Mungu
- Onyesha uongozi wa kitumishi unaofananana ule wa Kristo.
- Onyesha huruma, ukarimu na msamaha katika mahusiano yote (wakiwemo watu wenye mahitaji maalum).
- Kufariji na kusaidia wengine wakati wa shida (yaani kifo, shida za ndoa, ugonjwa, n.k.).
- Wasaidie watu wanaotegemea kuoana kujiandaa kwa ajili ya ndoa yao.
- Kujihusisha wenyewe katika huduma kwa, watoto na vijana.
- Eleza majukumu ya waume na wake katika kukuza uaminifu na upendo katika ndoa na familia.
- Eleza athari za akina baba watoro.
- Suluhisha migogoro katika mahusiano.